Guardiola: nakaribia kustaafu kufundisha soka



Guardiola amezifundisha klabu za Barcelona na Bayern Munich kwa mafanikio makubwa
Image captionGuardiola amezifundisha klabu za Barcelona na Bayern Munich kwa mafanikio makubwa

Meneja wa Manchester City Pep Guardiola anakaribia kustaafu kufundisha soka na hataitakuwa miaka 65 kama alivyodhani awali.
Muispania huyo amewahi kuifundisha klabu ya Barcelona ka mafanikio makubwa kisha Bayern Munich kabla ya kuchukua nafasi ya Manuel Pellegrini Man city.
''Nitakuwa hapa Manchester kwa misimu ama mitatu labda na zaidi,'' Guardiola mwenye miaka 45 alisema kabla ya ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Burnley.
''Sitakaa kwenye benchi mpaka miaka 60-65.Nafikiri mchakato wa kuanza kusema kwaheri umekaribia.
Guardiola ameshinda vikombe 14 katika miaka minne akiwa na Barcelona, ikiwa ni pamoja na vikombe vitatu vya La Liga na viwili vya ligi ya mabingwa Ulaya.
Alipumzika mwaka mzima kabla ya kujiunga na Bayern Munich na kuwaongoza kupata vikombe vitatu vya ligi kuu licha ya kukosa ligi ya mabingwa Ulaya
Kikosi cha Guardiola kilicheza pungufu baada ya Fernandinho kupewa kadi nyekundu lakini magoli ya Gael Clichy na Sergio Aguero yaliwapa ushindi. Source BBC swahili. 

Comments