Rais wa Mexico amrejesha waziri aliyemtimua





Rais Enrique Pena Nieto
Image captionRais Enrique Pena Nieto

Rais wa Mexico Enrique Pena Nieto, amemteua waziri wa zamani wa fedha Luis Videgaray kuwa waziri wa mambo ya nje.
Awali Luis alifutwa kazi kufuatia ziara nchini Marekani muda mfupi baada ya kuteuliwa kwa Donald Trump.
Akizungumzia uteuzi huo huo wa waziri aliyekuwa amemfukuza kazi,Rais Nieto anasema amechukua hatua ili kupitia waziri huo mpya wa mambo ya nje kuweza kuimarisha mahusiano na ujio wa Rais wa Marekani Donald Trump

Comments